The Noble Qur'an Encyclopedia
Towards providing reliable exegeses and translations of the meanings of the Noble Qur'an in the world languagesThe Traducer [Al-Humaza] - Swahili translation - Ali Muhsen Al-Berwani
Surah The Traducer [Al-Humaza] Ayah 9 Location Maccah Number 104
Ole wake kila safihi, msengenyaji! [1]
Aliye kusanya mali na kuyahisabu. [2]
Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele! [3]
Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama. [4]
Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama? [5]
Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa. [6]
Ambao unapanda nyoyoni. [7]
Hakika huo utafungiwa nao [8]
Kwenye nguzo zilio nyooshwa. [9]