عربيEnglish

The Noble Qur'an Encyclopedia

Towards providing reliable exegeses and translations of the meanings of the Noble Qur'an in the world languages

Stoneland, Rock city, Al-Hijr valley [Al-Hijr] - Swahili translation - Ali Muhsen Al-Berwani

Surah Stoneland, Rock city, Al-Hijr valley [Al-Hijr] Ayah 99 Location Maccah Number 15

Alif Lam Ra. (A.L.R). Hizi ni Aya za Kitabu na Qur'ani inayo bainisha. [1]

Hakika Sisi ndio tulio teremsha Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio tutao ulinda. [9]

Hawayaamini haya, na hali ya kuwa umekwisha wapitia mfano wa watu wa kale. [13]

Isipo kuwa mwenye kusikiliza kwa kuibia, naye hufuatwa na kijinga cha moto kinacho onekana. [18]

Na tumekujaalieni humo vitu vya maisha yenu, na ya hao ambao nyinyi sio wenye kuwaruzuku. [20]

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye atakaye wakusanya. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mjuzi. [25]

Na Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura. [28]

(Mwenyezi Mungu) akasema: Ewe Iblisi! Una nini hata hukuwa pamoja na walio sujudu? [32]

(Mwenyezi Mungu) akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe ni maluuni! [34]

Akasema (Iblisi): Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watapofufuliwa. [36]

(Mwenyezi Mungu) akasema: Hakika wewe ni katika walio pewa muhula [37]

Na bila shaka Jahannamu ndipo pahali pao walipo ahidiwa wote. [43]

Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem. [45]

(Wataambiwa:) Ingieni kwa salama na amani. [46]

Waambie waja wangu ya kwamba Mimi ndiye Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu. [49]

Akasema: Na nani anaye kata tamaa na rehema ya Mola wake Mlezi ila wale walio potea? [56]

Isipo kuwa walio mfuata Luut'i. Bila ya shaka sisi tutawaokoa hao wote. [59]

Alisema (Luut'i): Hakika nyinyi ni watu msio juulikana. [62]

Akasema: (Luut'i) Hakika hawa wageni wangu, basi msinifedheheshe. [68]

Naapa kwa umri wako! Hakika hao walikuwa katika ulevi wao, wakihangaika ovyo. [72]

Na miji hii ipo kwenye njia inayo pitiwa. [76]

Hakika Sisi tunatosha kukukinga na wanao kejeli. [95]

Na Sisi tunajua kwa hakika kuwa wewe kifua chako kinaona dhiki kwa hayo wayasemayo. [97]

Basi mtakase Mola wako Mlezi kwa kumhimidi, na uwe miongoni wanaomsujudia. [98]

Na muabudu Mola wako Mlezi mpaka ikufikie Yakini. (nao ni Mauti) [99]