عربيEnglish

The Noble Qur'an Encyclopedia

Towards providing reliable exegeses and translations of the meanings of the Noble Qur'an in the world languages

Ya Seen [Ya Seen] - Swahili translation - Ali Muhsen Al-Berwani

Surah Ya Seen [Ya Seen] Ayah 83 Location Maccah Number 36

Ya-Sin (Y.S.). [1]

Kwa Haki ya Qur'ani yenye hikima! [2]

Hakika wewe ni miongoni mwa walio tumwa! [3]

Uteremsho wa Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu. [5]

Ili uwaonye watu ambao baba zao hawakuonywa , basi wao wamekuwa wenye kughafilika. [6]

Bila ya shaka kauli imekwisha thibiti juu ya wengi katika wao, kwa hivyo hawaamini. [7]

Wakasema: Ukorofi wenu mnao wenyewe! Je! Ni kwa kuwa mnakumbushwa? Ama nyinyi ni watu walio pindukia mipaka. [19]

Basi hakika mimi hapo nitakuwa katika upotovu ulio dhaahiri. [24]

Hakika mimi nimemuamini Mola wenu Mlezi, basi nisikilizeni! [25]

Jinsi Mola wangu Mlezi alivyo nisamehe, na akanifanya miongoni mwa walio hishimiwa. [27]

Watapata humo kila namna ya matunda na watapata kila watakacho kitaka. [57]

"Salama!" Hiyo ndiyo kauli itokayo kwa Mola Mlezi Mwenye kurehemu. [58]

Wala hatukumfundisha (Muhammad) mashairi, wala hayatakikani kwake hayo. Haukuwa huu ila ni ukumbusho na Qur'ani inayo bainisha. [69]

Na Sisi tukawadhalilishia. Basi baadhi yao wako wanao wapanda, na baadhi yao wanawala. [72]

Kwani mwanaadamu haoni ya kwamba Sisi tumemuumba yeye kutokana na tone la manii? Kisha sasa yeye ndio amekuwa ndiye mgomvi wa dhaahiri! [77]

Na akatupigia mfano, na akasahau kuumbwa kwake, akasema: Ni nani huyo atakaye ihuisha mifupa nayo imekwisha mung'unyika? [78]