عربيEnglish

The Noble Qur'an Encyclopedia

Towards providing reliable exegeses and translations of the meanings of the Noble Qur'an in the world languages

Those who set the ranks [As-Saaffat] - Swahili translation - Ali Muhsen Al-Berwani

Surah Those who set the ranks [As-Saaffat] Ayah 182 Location Maccah Number 37

Naapa kwa wanao jipanga kwa safu. [1]

Na kwa wenye kusoma Ukumbusho. [3]

Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja. [4]

Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara. [10]

Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara. [12]

Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri. [15]

Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini. [29]

Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu. [31]

Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu. [32]

Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja. [33]

Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu? [36]

Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa. [40]

Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem. [45]

Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri. [48]

Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika. [49]

Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa na rafiki. [51]

Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki. [52]

Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa. [57]

Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa walio dhulumu. [63]

Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashet'ani. [65]

Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji yamoto yaliyo chemka. [67]

Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu. [68]

Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliokhitariwa. [74]

Na tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja baadaye. [78]

Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema. [80]

Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu? [86]

Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote? [87]

Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa! [89]

Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe [95]

Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya! [96]

Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa. [99]

Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema. [100]

Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji. [103]

Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu. [107]

Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye. [108]

Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema. [110]

Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema. [112]

Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume. [123]

Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?. [126]

Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa;. [127]

Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa. [128]

Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa walio kuja baadaye. [129]

Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume. [133]

Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma. [135]

Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa. [141]

Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa. [142]

Na ingeli kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Mwenyezi Mungu,. [143]

Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?. [149]

Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!. [152]

Subhana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo msingizia. [159]

Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa. [160]

Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu. [165]

Na hakika sisi ndio wenye kusabihi kutakasa. [166]

Na walikuwapo walio kuwa wakisema:. [167]

Bila ya shaka tungeli kuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye ikhlasi. [169]

Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakao nusuriwa. [172]

Subhana Rabbi'l'Izzat Ametakasika Mola Mlezi Mwenye enzi na yale wanayo mzulia. [180]

Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote. [182]