عربيEnglish

The Noble Qur'an Encyclopedia

Towards providing reliable exegeses and translations of the meanings of the Noble Qur'an in the world languages

The winnowing winds [Adh-Dhariyat] - Swahili translation - Ali Muhsen Al-Berwani

Surah The winnowing winds [Adh-Dhariyat] Ayah 60 Location Maccah Number 51

Naapa kwa pepo zinazo tawanya! [1]

Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka ni kweli! [5]

Na kwa hakika malipo bila ya shaka yatatokea. [6]

Hakika nyinyi bila ya shaka mmo katika kauli inayo khitalifiana. [8]

Anageuzwa kutokana na haki mwenye kugeuzwa. [9]

Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem. [15]

Akahisi kuwaogopa katika nafsi yake. Wakasema: Usiwe na khofu, nao wakambashiria kupata kijana mwenye ilimu. [28]

Ndipo mkewe akawaelekea, na huku anasema na akijipiga usoni kwa mastaajabu, na kusema: Mimi ni kikongwe na tasa! [29]

Wakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyo sema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mwenye kujua. [30]

Yaliyo tiwa alama kutoka kwa Mola wako Mlezi kwa ajili ya wanao pindukia mipaka. [34]

Lakini alipuuza kwa sababu ya nguvu zake na akasema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu! [39]

Basi tukamkamata yeye na majeshi yake na tukawatupa baharini, na yeye ndiye wa kulaumiwa. [40]

Na katika khabari za Thamudi walipo ambiwa: Jifurahisheni kwa muda mdogo tu. [43]

Na mbingu tumezifanya kwa nguvu na uwezo na hakika Sisi bila ya shaka ndio twenye uwezo wa kuzitanua. [47]

Na ardhi tumeitandaza; basi watandazaji wazuri namna gani Sisi! [48]

Basi kimbilieni kwa Mwenyezi Mungu, hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake. [50]

Wala msifanye kuwa kuna mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake. [51]

Na sitaki kwao riziki, wala sitaki wanilishe.Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti. [57]