عربيEnglish

The Noble Qur'an Encyclopedia

Towards providing reliable exegeses and translations of the meanings of the Noble Qur'an in the world languages

Mount Sinai [At-tur] - Swahili translation - Ali Muhsen Al-Berwani

Surah Mount Sinai [At-tur] Ayah 49 Location Maccah Number 52

Naapa kwa mlima wa T'ur! [1]

Na Kitabu kilicho andikwa . [2]

Katika ngozi iliyo kunjuliwa! [3]

Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea. [7]

Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa. [10]

Watakuwa wameegemea juu ya viti vya enzi vilivyo pangwa kwa safu. Na tutawaoza mahuru-l-aini. [20]

Watapeana humo bilauri zisio na vinywaji vya kuleta maneno ya upuuzi wala dhambi. [23]

Basi Mwenyezi Mungu akatufanyia hisani na akatulinda na adhabu ya upepo wa Moto. [27]

Hakika sisi zamani tulikuwa tukimwomba Yeye tu. Hakika Yeye ndiye Mwema Mwenye kurehemu. [28]

Basi kumbusha! Kwani wewe, kwa neema ya Mola wako Mlezi, si kuhani wala mwendawazimu. [29]

Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji? [35]

Au Yeye Mwenyezi Mungu ana wasichana, na nyinyi ndio mna wavulana? [39]

Au wanae mungu asiye kuwa Mwenyezi Mungu? Subhanallah! Ametaksika Mwenyezi Mungu na hao wanao washirikisha naye. [43]

Na ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi. Kwani wewe hakika uko mbele ya macho yetu, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi unapo simama, [48]