عربيEnglish

The Noble Qur'an Encyclopedia

Towards providing reliable exegeses and translations of the meanings of the Noble Qur'an in the world languages

The Star [An-Najm] - Swahili translation - Ali Muhsen Al-Berwani

Surah The Star [An-Najm] Ayah 62 Location Maccah Number 53

Hayakuwa haya ila ni ufunuo ulio funuliwa; . [4]

Kisha akakaribia na akateremka. [8]

Akawa ni kama baina ya mipinde miwili, au karibu zaidi. [9]

Akamfunulia mja wake (Mwenyezi Mungu) alicho mfunulia. [10]

Karibu yake ndiyo ipo Bustani inayo kaliwa. [15]

Kilipo ufunika huo Mkunazi hicho kilicho ufunuika. [16]

Jicho halikuhangaika wala halikuruka mpaka. [17]

Kwa yakini aliona katika Ishara kubwa kabisa za Mola wake Mlezi. [18]

Je! Nyinyi mnao wana wanaume na Yeye ndio awe na wanawake? [21]

Ati mtu anakipata kila anacho kitamani? [24]

Mwenyezi Mungu tu ndiye Mwenye dunia na Akhera. [25]

Ya kwamba hakika nafsi iliyo beba madhambi haibebi madhambi ya mwengine? [38]

Na kwamba Yeye ndiye anaye leta kicheko na kilio. [43]

Na kwamba Yeye ndiye anaye fisha na kuhuisha. [44]

Kutokana na mbegu ya uzazi inapo miminwa. [46]

Na kwamba ni Yeye ndiye anaye tosheleza na kukinaisha. [48]

Na kwamba hakika Yeye ndiye Mola Mlezi wa nyota ya Shii'ra. [49]

Na kwamba Yeye ndiye aliye waangamiza A'di wa kwanza, [50]

Na miji iliyo pinduliwa, ni Yeye aliye ipindua. [53]

Basi neema gani ya Mola wako Mlezi unayo ifanyia shaka? [55]