عربيEnglish

The Noble Qur'an Encyclopedia

Towards providing reliable exegeses and translations of the meanings of the Noble Qur'an in the world languages

The Event, The Inevitable [Al-Waqia] - Swahili translation - Ali Muhsen Al-Berwani

Surah The Event, The Inevitable [Al-Waqia] Ayah 96 Location Maccah Number 56

Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa. [15]

Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi. [18]

Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa. [19]

Katika mikunazi isiyo na miba, [28]

Na migomba iliyo pangiliwa, [29]

Na kivuli kilicho tanda, [30]

Na matandiko yaliyo nyanyuliwa. [34]

Wanapendana na waume zao, hirimu moja. [37]

Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka, [42]

Si cha kuburudisha wala kustarehesha. [44]

Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa. [45]

Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu. [55]

Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza? [58]

Mkisema: Hakika sisi tumegharimika; [66]

Je! Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha? [69]

Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu. [74]

Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua! [76]

Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu, [77]

Katika Kitabu kilicho hifadhiwa. [78]

Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote. [80]

Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha? [82]

Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli? [87]

Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema. [89]

Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia. [91]

Basi karamu yake ni maji yanayo chemka, [93]

Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa. [96]