عربيEnglish

The Noble Qur'an Encyclopedia

Towards providing reliable exegeses and translations of the meanings of the Noble Qur'an in the world languages

The Pen [Al-Qalam] - Swahili translation - Ali Muhsen Al-Berwani

Surah The Pen [Al-Qalam] Ayah 52 Location Maccah Number 68

Nuun. Naapa kwa kalamu na yale wayaandikayo! [1]

Ni nani kati yenu aliye pandwa na wazimu. [6]

Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliye ipotea Njia yake, na Yeye ndiye anaye wajua zaidi walio ongoka. [7]

Wanatamani lau unge lainisha ili nao wakulainishie. [9]

Wala usimt'ii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa, [10]

Mwenye kuzuia kheri, dhaalimu, mwingi wa madhambi, [12]

Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu. [13]

Wala hawakusema: Mungu akipenda! [18]

Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo. [25]

Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu. [29]

Asaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi. [32]

Waulize: Ni nani miongoni mwao dhamini wa haya? [40]

Na ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara. [45]

Kama isingeli mfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angeli tupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa. [49]

Lakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema. [50]

Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote. [52]