عربيEnglish

The Noble Qur'an Encyclopedia

Towards providing reliable exegeses and translations of the meanings of the Noble Qur'an in the world languages

The reality [Al-Haaqqa] - Swahili translation - Ali Muhsen Al-Berwani

Surah The reality [Al-Haaqqa] Ayah 52 Location Maccah Number 69

Nini hilo Tukio la haki? [2]

Na nini kitakujuulisha nini hilo Tukio la haki? [3]

Wakamuasi Mtume wa Mola wao Mlezi, ndipo Yeye Mola akawakamata kwa mkamato ulio zidi nguvu. [10]

Ili tuyafanye hayo kuwa ni waadhi kwenu na kila sikio linalo sikia liyahifadhi. [12]

Basi yeye atakuwa katika maisha ya kupendeza, [21]

Na ama atakaye pewa kitabu chake katika mkono wake wa kushoto, basi yeye atasema: Laiti nisingeli pewa kitabu changu! [25]

Wala nisingeli jua nini hisabu yangu. [26]

Laiti mauti ndiyo yangeli kuwa ya kunimaliza kabisa. [27]

(Pasemwe): Mshikeni! Mtieni pingu! [30]

Wala hana chakula ila usaha wa watu wa Motoni. [36]

Kwa hakika hii ni kauli iliyo letwa na Mjumbe mwenye hishima. [40]

Ni uteremsho utokao kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote. [43]

Bila ya shaka tungeli mshika kwa mkono wa kulia, [45]

Kisha kwa hakika tungeli mkata mshipa mkubwa wa moyo! [46]

Na hapana yeyote katika nyinyi ambaye angeli weza kutuzuia. [47]

Na hakika Sisi bila ya shaka tunajua kwamba miongoni mwenu wapo wanao kadhibisha. [49]

Na hakika bila ya shaka itakuwa ni majuto kwa wanao kataa. [50]

Na hakika hii bila ya shaka ni haki ya yakini. [51]

Basi litakase jina la Mola wako Mlezi Mtukufu. [52]