عربيEnglish

The Noble Qur'an Encyclopedia

Towards providing reliable exegeses and translations of the meanings of the Noble Qur'an in the world languages

The Ascending stairways [Al-Maarij] - Swahili translation - Ali Muhsen Al-Berwani

Surah The Ascending stairways [Al-Maarij] Ayah 44 Location Maccah Number 70

Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea! [1]

Kwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia . [2]

Kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja. [3]

Basi subiri kwa subira njema.Hakika wao wanaiona iko mbali! [5]

Na Sisi tunaiona iko karibu. [7]

Siku ambayo mbingu zitakapo kuwa kama maadeni iliyo yayushwa. [8]

Ijapo kuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe, [11]

La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa, [15]

Utamwita kila aliye geuza mgongo na akageuka. [17]

Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi. [18]

Kwa mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba; [25]

Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo. [28]

Makundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto! [37]