عربيEnglish

The Noble Qur'an Encyclopedia

Towards providing reliable exegeses and translations of the meanings of the Noble Qur'an in the world languages

The rising of the dead [Al-Qiyama] - Swahili translation - Ali Muhsen Al-Berwani

Surah The rising of the dead [Al-Qiyama] Ayah 40 Location Maccah Number 75

Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake! [4]

Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake. [5]

La! Hapana pa kukimbilia! [11]

Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani, [20]

Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana. [24]

Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo. [25]

La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo, [26]

Na pakasemwa: Nani wa kumganga? [27]

Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki; [28]

Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi! [30]

Kwa sababu hakusadiki, wala hakuswali. [31]

Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo. [38]