عربيEnglish

The Noble Qur'an Encyclopedia

Towards providing reliable exegeses and translations of the meanings of the Noble Qur'an in the world languages

Those who drag forth [An-Naziat] - Swahili translation - Ali Muhsen Al-Berwani

Surah Those who drag forth [An-Naziat] Ayah 46 Location Maccah Number 79

Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu! [1]

Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka! [6]

Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano! [14]

Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia: [16]

Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha. [19]

Lakini aliikadhibisha na akaasi. [21]

Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi. [22]

Akakusanya watu akanadi. [23]

Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa. [24]

Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo. [25]

Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga! [27]

Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri. [28]

Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake [29]

Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona, [36]

Basi ama yule aliye zidi ujeuri, [37]

Na ama yule anaye ogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio, [40]

Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake. [44]

Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuikhofu. [45]