عربيEnglish

The Noble Qur'an Encyclopedia

Towards providing reliable exegeses and translations of the meanings of the Noble Qur'an in the world languages

The Sun [Ash-Shams] - Swahili translation - Ali Muhsen Al-Berwani

Surah The Sun [Ash-Shams] Ayah 15 Location Maccah Number 91

Naapa kwa jua na mwangaza wake! [1]

Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza! [6]

Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza! [7]

Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotofu wao, [11]

Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake. [13]

Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa. [14]

Wala Yeye haogopi matokeo yake. [15]